Mchuano mkuu unaoleta timu bora zaidi za Kilimanjaro
Angalia Mechi za LeoTimu zizizofuzu hatua ya makundi kupata muda wa kujinoa kwa ajili ya mtoano wa hatua ya 16 Bora ya mashindano ya Zuberi Cup Tournament
Vilabu vyote kupata nafasi ya kufanya usajili wa wachezaji watano watakaochuana kwenye hatua ya 16 bora ya mashindano haya ya Zuberi Cup.
La Familia FC wakiendelea kuonyesha ukongwe wao kwenye mashindano haya huku akitambia mashabiki wa Msaranga FC
Uwanja wa Railway ndio uwanja mkuu unaotumika kwa mechi za muhimu za Zuberi Cup. Uwanja huu una uwezo wa kuwashika watu 1000 na umekarabatiwa hivi karibuni ili kuwa na viwango vya kimataifa. Uwanja huu ni wa khistoria na umeshashuhudia mechi nyingi za kumbukumbu.
Mabango yaliyopo kwenye uwanja mkuu wa mashindano ya Zuberi Cup yanayomuonyesha Mhe. Dkt. Samia Suluhu akiwa na Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo. Meya ni mpenda michezo na mdhamini mkuu wa mchuano wa Zuberi Cup ambao unalenga kuendeleza talanta za vijana.